Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa jana ilitoa taarifa na kueleza kuwa uvamizi wa kijeshi wa Saudi Arabia huko Yemen na uharibifu na kusisitiza kuwa jinai zinazofanywa na utawala wa Aal Saudia zimewasababishia watoto wa Yemen kukumbwa na mgogoro mkubwa zaidi wa chakula dunia na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.
Ofisi hiyo ya Umoja wa Mataifa imeeleza kuwa watoto milioni 11 wa Yemen wanahitaji misaada ya haraka ya kibinadamu. Taarifa ya Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa imeongeza kuwa hakuna uwezekano wowote wa kupatikana huduma za tiba za msingi na chakula huko Yemen na kwamba watoto nchini humo hawana uwezo wa kujidhaminia mahitaji yao.
Taarifa ya Ofisi ya Uratibu wa Misaada ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa imeashiria pia mustakbali usiojulikana wa mamilioni yha wanafgunzi wa malefu ya walimu huko Yemen na kusisitiza mfumo wa elimu chini humo unakaribia kusambaratika.
Wanafunzi zaidi ya milioni tano wanakabiliwa na hatari ya kushindwa kuendelea na masomo.
Saudi Arabia huku ikiungwa mkona na Marekani mwezi Machi mwaka 2015 ilianzisha uvamizi wa kijeshi huko Yemen na kuweka mzingiro wa nchi kavu, baharini na anga dhidi ya nchi hiyo kwa kisingizio cha kutaka kumrejesha madarakani kibaraka wake Rais mstaafu wa Yemen Abdu Rabuh Mansour Hadi.
No comments:
Post a Comment