Wednesday, September 27, 2017

27 September 2017, Wanawake nchini Saudia Arabia wataanza rasmi kuendesha magari 2018

Mwanamke wa Saudia katika kampeni ya kukaidi wanawake kutoendesha magari.

Saudi Arabia itawaruhusu kwa mara ya kwanza wanawake kuendesha magari kwa mujibu wa amri iliyotolewa na mfalme wa nchi hiyo.

Vyombo vya habari vimeripoti Jumanne kuhusu amri hiyo ya kifalme ambayo inataka leseni za kuendesha magari zitolewe kwa wote wanaume na wanawake.

Aidha nchini  hio sasa ndio  nchi pekee ambapo inawazuia wanawake kuendesha magari.

Shirika la habari la Saudi Arabia -SPA limeripoti kuwa amri hiyo itaanza kutumika rasmi mwezi Juni mwaka 2018.

No comments: