Ujerumani wameanza kuelekea kwenye masanduku ya kupigia kura hii leo katika uchaguzi wa taifa ambao unatazamiwa kumpa ushindi kwa muhula wa nne Bi Angela Merkel kama Kansela wa nchi hiyo.
Vituo vya kupigia kura vimefunguliwa leo asubuhi kuanzia saa mbili na vitakuwa wazi hadi jioni saa 12 kwa majira ya Ujerumani. Raia wasiopungua milioni 61. 5 waliotimiza masharti ya kupiga kura wanashiriki katika uchaguzi wa leo.
Kansela wa Ujerumani anagombea nfasi hiyo kwa muhula wa nne huku akijaribu kuhifadhi nafasi ya chama chake cha Christian Democrat (CDU), ambacho kinatambulika kama kundi kubwa zaidi katika bunge la taifa la Ujerumani, "The Bundestag."
Katika uchaguzi wa leo, Angela Merkel anachuana vikali na Martin Schulz ambaye ni kiongozi wa chama cha Social Democrats cha mrengo wa kushoto-kati (SPD) ambaye ni mkuu wa zamani wa bunge la Ulaya.
No comments:
Post a Comment