Tuesday, August 29, 2017

29 August 2017, Polisi yachunguza upya kifo cha mchora katuni Naji

Polisi wa Uingereza wamesema wanachunguza tena mauaji ya mchora Katuni wa Kipalestina Naji Al-Ali.

Alipigwa risasi wakati alipokuwa akitembea kuelekea ofisini kwake jijini London Julai 1997.

Naji al- Ali anajulikana zaidi kutokana na katuni zake ambazo zilikuwa zikichapishwa katika gazeti la Kuwaiti, na mara kadhaa alikuwa akiwashutumu viongozi wa Kiarabu na utawala.

Polisi wa mji wa London wamesema wanamatumaini kwamba watu ambao hawakutaka kuzungumza wakati mauaji yalipotokea pengine sasa wataweza kuzungumza.

No comments: