Rais wa Uturuki Recep Tayyıp Erdoğan ametoa wito kwa mataifa ya kiislamu kuongeza ushirikiano baina yao .
Erdoğan alisema haya akiwa ziarani Jordan katika mji mkuu wa Amman kuadhimisha miaka 70 ya uhusiano wa kidiplomasia baina ya Uturuki na Jordan .
Rais Erdoğan alifahamisha haya akiwa katika mkutano na wajumbe kutoka nchi hizo mbili katika ikulu ya Hussainiah Palace na kusema kuwa kipindi hiki ulimwengu wa kiislamu unapitia wakati mgumu .
Aliendelea usisitiza kwamba ni nyakati hizi ambazo waislamu wanatakiwa kuongeza ushirikiano baina yao .
Awali siku ya Jumatatu rais Erdoğan alikutana na mfalme Abdullah wa Jordan na kuzumgumza kuhusu matukio na mzozo baina ya Israel na Palestina .
Mfalme Abdullah alitoa shukrani za dhati kwa Erdoğan kwa kuendelea kuunga mkono Jordan na pia msimamo wake kuhusu suala la Al Aqsa .
Erdoğan aliahidi kuendelea kushirikiana na Jordan katika juhudi za kulinda hadhi ya mskiti wa Al Aqsa .
No comments:
Post a Comment