Monday, July 31, 2017

31 july 2017, Serikali kumaliza adha ya maji Mbeya

Serikali imedhamiria kumaliza tatizo la upatikanaji majisafina salama katika maeneo mbalimbali nchiniikiwemo wilaya ya Rungwe mkoaniMbeya ambayo imetengewa sh.bilioni2.72kwa ajiliya ujenziwa miradiya maji.

Kaulihiyo imetolewa na WaziriMkuu Kassim Majaliwa wakatiakizungumza kwa nyakatitofauti na wananchiwa Halmashauriza Rungwe na Busokelo katika mikutano ya hadhara aliyoifanya Kandete na Tandale mkoaniMbeya.

WaziriMkuu amesema mkakatihuo unatekelezwa kupitia Kampeniya Rais Dkt.John Magufuliya kumtua mama ndoo kichwani,wananchikatika maeneo yote nchiniwatapata huduma ya maji safina salama katika umbaliusiozidimita 400 kutoka kwenye makaziyao.

WaziriMkuu alitaja mradimwingine unaotekelezwa wilayaniRungwe kuwa nipamoja na mradiwa majiwa Masoko wenye thamaniya sh.bilioni5.3,utakaohudumia jumla ya vijiji15. “Mradihuu nimiongonimwa miradiinayojengwa chiniya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji kwa fedha za ndani.” alisema WaziriMkuu.

Mradihuo utakapokamilika utawanufaisha wananchiwapatao 19,624katika vijijivya Bulongwe,Ngaseke,Igembe,Ntandabala, Lupando,Bujesi,Lufumbi,Nsyasa,Ikama,Itagata, Busisya,Mbaka,Isabula,Lwifa na Nsanga.

No comments: