Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Mbwana Ally Samatta jana Jumamosi alikuwa na kibarua cha kuitumikia timu yake ya KRC Genk katika mechi yao ya kwanza wa Ligi Kuu Ubelgiji msimu wa 2017/18 dhidi ya Waasland Beveren.
Samatta aliifungia timu yake goli la pili katika dakika ya 80 na kutoa 'assist' ya goli la 3 ambapo lilifanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya 3-3.
Magoli ya Genk yakifungwa na Jose Naranjo dakika ya 70, Mbwana Samatta dakika ya 80 na dakika ya 82 Shrivjers akafunga goli la mwisho.
Klabu ya KRC Genk ilicheza game yake ya kwanza katika uwanja wake wa nyumbani dhidi ya Waasland Beveren na kulazimishwa sare hiyo ya kufungana magoli 3-3.
No comments:
Post a Comment