Friday, July 28, 2017

28 july 2017, Kundi la Boko Haramu lateka wafanyakazi wa shirika la mafuta Nigeria

Shirika la mafuta linaliomilikiwa na serikali nchini Nigeria limetangaza kuwa baadhi ya wafanyakazi wake wametekwa na kundi la kigaidi la Boko Haram na hawajulikani walipo mpaka sasa.

Shirika la mafuta linaliomilikiwa na serikali nchini Nigeria limetangaza kuwa baadhi ya wafanyakazi wake wametekwa na kundi la kigaidi la Boko Haram na hawajulikani walipo mpaka sasa.

Ripoti hio imetolewa baada ya Boko Haramu kuvamia na kuua baadhi ya wafanyakazi katika eneo la Gubio siku mbili zilizopita.

Kwa mujibu wa habari,kati ya waliotekwa ni askari saba waliokuwa katika operesheni ya kukomboa watu.

Watu 48 wameripotiwa kuuawa wakiwemo askari,wafanyakazi wa shirika la mafuta ambao miili yao imefikishwa katika hospitali ya Maiduguri.

Mwenyekiti wa kampuni hiyo ya mafuta NNPC amesema kuwa uchunguzi utaendelea endapo kutakuwa na uhakika wa ulinzi bora na usalama.

Hata hivyo mkuu wa majeshi Tukur Buratai,wiki iliyopita aliagiza wanajeshi kumsaka mkuu wa Boko Haramu Abubakar Shekau ndani ya siku arobaini.

No comments: