Liverpool wameandaa mkataba wa miaka
mitatu kwa ajili ya mchezaji wa safu ya kati wa Manchester United
Mbelgiji Marouane Fellaini, huku Paris St-Germain na Monaco pia
wakionyesha kumtaka kijana huyo mwenye umri wa miaka 30 ambaye mkataba
wake katika Old Trafford unamalizika mwisho wa msimu. (L'Equipe -kwa
Kifaransa)
Mkuu wa zamani wa waamuzi England Keith Hackett haelewi ni kwa nini Martin Atkinson hakumfukuza wuanjani beki wa Manchester United Ashley Young wakati wa mechi yao dhidi ya Manchester City. Amesema vitendo vya Atkinson ni thibitisho tosha ya kuonesha ni kwa nini waamuzi wa England waliachwa nje ya michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu. (Telegraph)
Meneja wa Chelsea Antonio Conte anasema klabu hiyo haistahili kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya iwapo haiwezi kuzishinda timu kama vile West Ham. Hii ni baada ya klabu hiyo kutoka sare ya 1-1 na West Ham. (Times)
No comments:
Post a Comment