Wednesday, August 23, 2017

23 August 2017, Lisu kupandishwa mahakamani

Mwanasheria wa Chadema na Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu amenyimwa dhamana baada ya kukamatwa leo kwa tuhuma za kumkashifu Rais John Magufuli na uchochezi.

Kwa mujibu wa  Mwananchi  mwanasheria wake Faraji Mangula amesema kwamba kesho Lissu atapandishwa mahakamani.

Amesema Polisi wamedai kwamba amemkashifu Rais a wakati wa mkutano wake na waandishi wa habari kwenye hoteli ya Protea.

‘’Polisi wamemnyima dhamana wamesema wanafanya utaratibu wakumfikisha mahakamani’’amesema.

No comments: