Tuesday, April 10, 2018

10 APRIL 2018,RAIA 9 WA CHINA WAKAMATWA KONGO KWA TUHUMA ZA KUCHIMBA MADINI

Raia 9 kutoka China  waripotiwa  kukamatwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wakituhumiwa kuchimba  madini Ituri bila ya kuwa na kibali. 
 Raia hao 9 kutoka China wamekuwa wakichimba madini bşla ya kibali Ituri tangu mwaka 2011.
Taarifa hiyo imetolewa  Jumapili  Mambasa Kaskazini-Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Msimamizi  katika kitengo kinachohusika na migodi na uchimbaji madini Ituri Deogratias Ombalia  amesema kuwa raia hao kutoka China wamekamatwa wakiwa hawana  kibali kinachowaruhusu kuendesha shughuli waliokuwa wakifanya Ituri. 
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni taifa barani Afrika lenye utajiri mkubwa wa madini huku raia wake wakiwa  katika hali mbaya ya umaskini.

No comments: